Juzi kwenye ukurasa wa Facebook wa mdogo wangu nilikutana na maelezo yasemayo "While individuals embrace each other in rural, they stay apart in Urban."
Kisha nikawaza kuwa MJINI NI WAPI? Nikaweka majibu kuwa "Hivi Mjini ni wapi? Nikiwa Nyakibale niliona Omuluhamila kama mjini. Kufika pale nikaona Kaagya kama mjini, Na Kaagya wanaona Kashozi kama mjini na wa Kashozi wanaona Bukoba Mjini ndio kumekucha. Aliye Bikoba mjini anaamini Mwanza ndio kwen...yewe (tena anywhere in Mwanza) na aliye Mwanza anaamini Arusha ama Dar ama etc ndio haswaaaaa. Aliye Dar Kibondemaji anaamini Kariako ndio mjini na wa Kariakoo anaangalia Masaki. Wa Masaki anatazama Nairobi na nje ya nchi hata Marekani na hata hapa Marekani kuna aliye DC ama Los Angeles na bado anautafuta mji. KWANI MJINI NI WAPI? Labda hata ndani a nyumba yenu kuna mjini ambapo ni Master bedroom na aliye humo naye anaamini choo cha humo ndimo mjini mwake. KWA MAANA NYINGINE, LABDA MJI NA KIJIJI NI FIKRA TU. Kwa kuwa anayekula raha sana duniani na kuamini ana kila kitu, anaambiw na kuwa KUNA MBINGUNI KULIKO NA MANONO KULIKO ANAYOPATA. Labda huko ndio MJINI. Lakini tukifia huko hatutaambiwa kuna "mji mwingine?" NAWAZA KWA SAUTI TUUUUUUU..."
Na bado nawaza..........MJINI NI WAPI?
No comments:
Post a Comment